Highlights

STARTING A BUISNESS AT YOUNG AGE and DEVELOPING ENTREPRENEURSHIP SPIRIT/KUANZA BIASHARA KATIKA UMRI MDOGO NA KUENDELEZA DHIMA YA UJASIRIAMALI.


STARTING A BUISNESS AT YOUNG AGE and DEVELOPING ENTREPRENEURSHIP SPIRIT/KUANZA BIASHARA KATIKA UMRI MDOGO NA KUENDELEZA DHIMA YA UJASIRIAMALI.
Nini maana ya Biashara ? zipo maana nyingi sana kama 
Biashara ni kitendo cha kununua na kuuza bidhaa mbalimbali
Biashara inaweza kuwa utekelezaji wa wazo fulani kwa namna ambayo unapata pesa katika hiyo
Biashara na ujasiriamali ni vitu viwili katika fungu moja 
 Mjasiriamali ni 
mtu anayechukua hatua za utekelezaji wa wazo kwa nia ya kupata fedha 
Mmiliki wa biashara anayefanya kazi huku akikabiliana na Changamoto mbali mbali kwa juhudi kubwa  (He takes initiatives dispite the Risk))
Mjasiriamali ni mtu anayekuwa tayari kuanzisha biashara na kuwa tayari kuwajibika kwa kila hali na yuko tayari kwa matokeo yoyote 
Ni mtu anayekuwa tayari kuanza upya hata biashara inapokwama na hata kufa kabisa anatulia anajitathmini kisha anaanza tena.

Na ujasiriamali ni kitendo cha kuchukua hatua na kisha kuanza hiyo biashara. Hasa kwa lengo la kupata fedha na kutatua matatizo ya watu.

KUTATUA MATATIZO YA WATU
KWANINI NI MUHIMU KUANZA BIASHARA AU UJASIRIAMALI KATIKA UMRI MDOGO.
Tunaona katika 
Maombolezo 3:27
Ni vema mwanadamu aichukue nira Wakati wa ujana wake.
Hivyo ni vyema kufanya maamuzi na kuanza katika ujana ili hata ukikutana na changamoto unakuwa na nafasi ya kuzitatua maana umri wako bado unakupa nafasi ya kufanya mambo mengi zaidi .Kumbuka NGUVU ZAKO NI MTAJI WAKO zitumie kwa hekima 
Ujasiriamali hausubiri umri fulani wala hauangalii jinsia Fulani, hivyo huna kikwazo cha kuanza sasa  amka chukua hatua.

 Mithali 20:29 
Fahari ya vijana ni nguvu zao, Na uzuri wa wazee ni kichwa chenye mvi.
kuna msemo unaosema 
WAKATI SAHIHI WA KUOTESHA MTI ULIKUWA MIAKA ISHIRINI ILIYOPITA....... WAKATI MWINGINE SAHIHI NI SASA.
(The best time to plant a tree was 20 years ago. The second best time is now)
Ukiwa kijana ni rahisi kujifunza maarifa na ujuzi kwa haraka zaidi kuliko ukiwa mzee .
Ukiwa na umri mdogo inakupa nafasi ya kuweza kushindana na ushindani wa soko la biashara husika maana kwa asilimia kubwa Utahusika moja kwa moja katika biashara yako.
Inaweza kukupa nafasi ya kuwa mgunduzi wa kwanza wa unachokifanya 
Inakupa nafasi ya kuwa mtoa ajira badala ya kuwa mtafuta ajira
Ukianza katika umri mdogo inakupa nafasi ya kustaafu mapema ukiwa bado una nguvu kwa sababu umeanza mapema na umewekeza vya kutosha kukutunza ukiwa mzee. 
Unaweza kujenga misingi mizuri ya familia na ngome ya nyumbani kwako mapema 


NAMNA YA KUANZA BIASHARA KATIKA UMRI MDOGO

v Challenge yourself
~Jiulize je ninaweza .??
~hivi ninapenda kujiajiri au kuajiriwa?
~hata kama nimeajiriwa ni vipi nitatengeneza kipato nje ya mshahara wangu?

v Engage your Gift / passion
Husisha karama yako au kile kitu unaona unapenda na unasikia amani ukikifanya na kinakupa furaha 
 *Turn your passion into profit*

v Take Risk
Mara nyingi tunaogopa kuanza kwa kuogopa matokeo ni wazi kuwa huwezi kuona matokeo bila kuamua kuanza,Jipe moyo mkuu ANZA LEO

v Believe in yourself
Vijana wengi tunakatishwa tamaa na maneno ya watu kwamba hatuwezi hatuwezi .Hebu leo ongea na nafsi yako jiambie NINAWEZA NA NINAYAWEZA YOTE KWAKUWA NINAE YESU ANAYENIPA UWEZO. Hii itakusaidia hata ukipata changamoto usikate tamaa maana STUMBLING BLOCKS ARE STEPING STONES

v Find the right association
Jihusianishe na watu husika kwa kile unachotaka kufanya Mfano. Ninataka kufungua Pharmacy watu husika ni walio kwenye mchepuo wa dawa au tiba kwa binadamu nikienda kuuliza changamoyo kwa watu wenye hoteli haitakuwa sahihi kwangu. Tafuta mkondo  sahihi wa uelekeo wa Wazo lako kisha anza.

v Have a mentor
Ni muhimu sana kuwa na mwangalizi ,Mwangalizi wa hali yako ya kiroho ila pia mwangalizi wa hali yako ya maisha na hatua zako , Na hakikisha unamwambia kwa uwazi kila unachoona anapaswa kujua .
atakusaidia , 
Atakushauri,
Atakufundisha,
Ataku councel,
Atakukosoa pia

Ila pia Mentor 
..Will help you to see Further
..Will help you to move faster
..Will help you to easy gain strength and overcome weakness
They are you are support base 
YOU NEED A MENTOR

 Wewe kama mjasiriamali inabidi uwe na uwezo wa kujiamini  kwasababu hatujapewa roho ya woga 
2 timotheo 1:7
Maana Mungu hakutupa roho ya woga, bali ya nguvu na ya upendo na ya moyo wa kiasi.
Wajasiriamali wengi tunaowaona hawakuanza moja kwa moja 
Walianza wakaanguka wakasimama wakaanza tena na leo tunawajua kwa majina NEVER GIVE UP 

Lazima mjasiriamali uwe na tabia ya kuwatia moyo wengine ili waweze kusimama kwasababu hata sisi tunaye aliyetuwezesha 
1 wakorinto 2:16
Maana, Ni nani aliyeifahamu nia ya Bwana, amwelimishe? Lakini sisi tunayo nia ya Kristo.

Kila unapotaka kuanza ukaona kama huwezi sema I HAVE THE MIND OF CHRIST ,mimi ninayo nia ya Kristo Hii itakupa ujasiri wa kusonga .Usisahau kabisa hili, mjasiriamali hachoki kutafuta maarifa na ujuzi hata atakapofanikiwa 
Mwanzo 26:18_25[18]Isaka akarudi akavichimbua vile visima vya maji walivyovichimba siku za Ibrahimu babaye; maana wale Wafilisti walikuwa wamevifukia baada ya kufa kwake Ibrahimu; naye akaviita majina kufuata majina alivyoviita babaye.[19]Watumwa wa Isaka wakachimba katika lile bonde, wakapata kisima cha maji yanayobubujika.[20]Wachungaji wa Gerari wakagombana na wachungaji wa Isaka wakisema, Maji haya ni yetu. Ndipo akakiita jina la kile kisima Eseki, kwa sababu waligombana naye.[21]Wakachimba kisima kingine, wakagombania na hicho tena. Akakiita jina lake Sitna. [22]Akaondoka huko akachimba kisima kingine, wala hicho hawakukigombania. Akakiita jina lake Rehobothi, akasema, Kwa kuwa sasa BWANA ametufanyia nafasi, nasi tutazidi katika nchi. [23]Akapanda kutoka hapo mpaka Beer-sheba.[24]BWANA akamtokea usiku uleule, akasema, Mimi ni Mungu wa Ibrahimu baba yako, usiogope, maana mimi ni pamoja nawe, nami nitakubarikia, na kuzidisha uzao wako kwa ajili ya Ibrahimu mtumishi wangu. [25]Akajenga madhabahu huko, akaliitia jina la BWANA. Akapiga hema yake huko, na watumwa wa Isaka wakachimba kisima huko.

Hivi ndivyo tunavyopaswa kuwa hakuna kukata tamaaa 
Ukishindwa leo unajaribu kesho,Ukikosa hivi inajaribu vile Usiwe na mipaka katika utendaji kwasababu UNAYAWEZA *YOTE* KATIKA YEYE ATUTIAYE NGUVU.Ukiona akili inakwambia inatosha sema hapana naweza kufanya tena kidogo hicho kidogo cha ziada kitaleta utofauti Ukikatishwa tamaa usijali, 
Sio lazima ukubalike sokoni moja kwa koja unachotakiwa kufanya ni 
KUWA WA TOFAUTI na UTOFAUTI Mfano. duka A na B wanauza mikate ila duka A... mikate yao huwa ni milaini na inahifadhiwa katika hali nzuri na safi Duka B...mikate yao ni migumu na inafungwa kwenye magazeti tuu yaliyotumika tayari.Wewe ukitaka mkate utaenda wapi??

 _Kuwa wa tofauti kwa kufanya kitu cha tofauti_
 Hivyo kijana wa Kikristo unapowaza kuwa mjasiriamali kumbuka UNAYO NIA YA KRISTO na kikubwa ni kumuhusisha katika kila jambo Kisha tulia fanya maamuzi sahihi, Sio kila wanachofanya wengine wakapata pesa unatakiwa ukifanye. 

YOU ARE IN A MISSION WITH CHRIST eee Kumbuka fedha yako ina sehemu utatoa Zaka ,Malimbuko,Fungu la kumi ,hivyo hakikisha unaipata kwa namna inayompendeza Mungu ili iwe manukato mbele zake .Turn your vision into a mission Ila pia hakikisha UNATOA SAPPORT KWA WAJASIRIAMALI WENGINE 

HITIMISHO 
Katika kuwaza kwako fikiria jambo kubwa ili ikishindikana ufanye kidogo chenye tija 

Ukiwaza kidogo ikashindikana basi utakosa kabisa cha kufanya.
( GO BIG OR GO HOME)

 An entrepreneur  dont  aim to play small 
 _Aim high reach higher_

Imetafsiriwa na Dada Vick Mcharo.



No comments