Highlights

MAISHA YA WOKOVU KWA KIJANA.






MAISHA YA WOKOVU KWA KIJANA.

Ninakusalimu katika jina la Bwana wetu Yesu Kristo.Ninapenda kumshukuru Mungu kwa kutupatia neema ya kujifunza somo hili ambalo limekuja kwa wakati sahihi la WOKOVU KWA VIJANA WAKRISTO. Miaka ya nyuma kidogo watu alikuwa wanaufahamu finyu au mdogo wa neno la Mungu na kwanzia mdogo hata mkubwa wote waliamini kuwa wokovu ulikuwa ni kwa ajili ya wazee ambao wanasubiria kuondoka duniani. Na hata kwenye baadhi ya nchi zilizoendelea katika nymba za ibada huwa wanaonekana wazee mara zote kuliko vijana na hii inatuonyesha dhahiri kuwa bado vijana hawajamfahamu muumba wao na hawajawekewa mazingira ya kujua kuwa imewapasa kuokoka wakati huu wakiwa bado wana nguvu na wasisubirie wakati wa uzee kwani hata uzee huo wanaweza wasiufikie ili kumpa Yesu maisha kama isemavyo 1Yohana 2;14b Ninawaandikia vijana kwa sababu mna nguvu ,na neno la Mungu linakaa ndani yenu,nanyi mmemshinda Yule mwovu

Neno la Mungu pia katika kitabu cha Muhubiri 12;1 bado linamtaka kijana kuwa karibu na Mungu na kuhakikisha anatumia nguvu zake kwa ajili ya kuujenga ufalme wa Mungu. Mkumbuke muumba wako siku za ujana wako,kabla hazijaja siku zilizo mbaya, wala hazijakaribia miaka utakaposema mimi sina furaha katika hiyo. Vijana tuna haja ya kumkumbuka muumba wetu wakati wa ujana na kumkumbuka Muumba wetu ni kwa kumpa Yesu kristo maisha, kuuishia wokovu na utakatifu.

MAMBO YA KUZINGATIA

1.KUMPOKEA NA KUMKUBALI YESU MAISHANI MWAKO.
Ni jambo la kwanza na la muhimu mno kumpokea Y esu Kristo kuwa mwokozi wako na mfalme ,rafiki ,mtetezi wako na awe namba moja katika maisha yako. Unapompokea Yesu Kristo maisha yako yatabadilishwa, marafiki ulionao watabadilika hata hali ya maisha uliyonayo itabadilishwa kabisa na Yesu ambae yupo ndani yako. Yohana 1;12 “Bali wote waliompokea aliwapa uwezo wa kuwa wana wa Mungu ndio wale waliaminio jina lake”.Na jambo la kushangaza huyu Yesu wetu alikufa kwa ajili yako na bado anayafuatilia maisha yako anakusubiri urudi kakwe nay eye yupo tiyari kukupokea jinsi ulivyo. Haijalishi umechafuka kiasi gani bado Bwana Yesu anataka na anahamu ukiri kwa kinywa chako na ufungue moyo wako akupokee neno la MUNGU katika Ufunuo 3;20 linasema “Tazama nasimama mlangoni nabisha ,mtu akiisikia sauti yangu na kuufungua mlango nitaingia kwake,nami nitakula pamoja naye na yeye pamoja nami”. Mungu anasema na wewe kwa namna ya hiyari kwa wakati huu. Ebu usije ukakipoteza kipindi hiki cha neema na ukaja wakati mbaya ambao utatamani kuokoka lakini utakuwa umeshachelewa sana,ebu angalia maisha unayoishi wewe kijana na ufanye uamuzi wa kumpa Yesu maisha yako.

2. KUMWAMINI YESU.
Baada ya kumpokea na kumpa nafasi Yesu kristo maishani mwako sasa unapaswa umwamini katika kitabu cha Yoh 1;12 tuliosoma hapo juu unasema“Bali wote waliompokea aliwapa uwezo wa kuwa wana wa Mungu ndio wale waliaminio jina lake”. Baada ya kumpokea na kupewa uwezo wa kuwa watoto wa Mungu neno la Mungu linasema ndio wale waliaminio neno lake. Bwana Yesu Kristo ndio neno lenyewe. Ukisoma yohana 1;1 na kuendelea . tunapaswa kumwamini Yeye na kumtegemea peke yake na kuacha miungu yoyote ile tuliyokuwa tukiiabudu au kuipa mafasi ya Mungu alliye hai maishani mwetu. Miungu hiyo inaweza kuwa wazazi wetu, marafiki , maisha ya mahusiano, ajira n.k kitu chochcote kile ulichokuwa unakipa nafasi ya kwanza badala ya Mungu .Tunapaswa kumoa Yesu nafasi yake anayostahili.  Yohana 3:16,” Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe wa pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele (wokovu) kuna kitu tunajifunza hapa, Kitu hicho ni lazima kuamini ndipo wokovu upatikane. Kwa sababu hiyo huwezi kupata wokovu pasipokumuamini Mungu na Yesu Kristo kama Bwana na Mwokozi wa maisha yako. Marko 16:16, Aaminiye na kubatizwa ataokoka; asiyeamini atahukumiwa .

 Waefeso 2;19 Basi tangu sasa ninyi si wageni wala wapitaji, bali ninyi ni wenyeji pamoja na watakatifu, watu wa nyumbani kwake Mungu. Ni maombi yangu umpe Yesu maisha ungali bado kijana.

1 comment: