Highlights

MAISHA YA KIJANA MKRISTO NA WOKOVU.




MAISHA YA KIJANA MKRISTO NA WOKOVU.
Ninakusalimu katika jina la Yesu Kristo Bwana wetu, juma lililopita tulipitia maisha ya wokovu ambapo tuliangalia mambo mawili ambayo ni ya muhimu ya kuzingatia ili kumpa Yesu maisha. Ambayo ni kumpokea na kumkubali Yesu kama mwokozi  wa maisha yako na Kumwamini Yesu kristo.
Siku ya leo ninatamani kuendelee mbele kidogo na kuangalia kwa kina ni mambo gani yanatokea pale mtu yeyete anapompokea Yesu kristo maishani mwake.


Roho mtakatifu anakaa ndani yako.
Roho mtakatifu ni nafsi ya tatu ya Mungu .Mungu ana nafsi tatu ambazo ni Mungu Baba, Mungu Mwana (Yesu kristo) na Mungu Roho mtakatifu. Baada ya Bwana Yesu kristo kukaa na wanafunzi wake baaada ya kufufuka aliwafundisha mambo mengi sana ambayo wangepaswa kuendelea kuyafanyia kazi ili ufalme wa Mungu uzidi kusonga mbele. Na kabla Yesu kupaa kwenda mbinguni aliwahaidi wanafunzi wake kuwapa msaidizi ambaye ni roho mtakatifu ambae atakuwa kiongozi na mwalimu kwao.Yohana 14; 16-18 Nami nitamwomba Baba baba naye atawapa msaidizi mwingine ili akae nanyi hata milele, ndiye roho wa kweli ambaye ulimwengu hauwezi kumpokea kwa sababu haumwoni wala haumtambui ;bali ninyi mnamtambua maana anakaa kwenu ,naye atakuwa ndani yenu. sitawaacha yatima naja kwenu.”Bwana Yesu asingeweza kuendelea kukaa na wanafunzi wake kwa muda wote kwani muda wake wa kukaa nao kimwili ulikuwa tiyari umeshaisha na alipaswa kurudi nyumbani kwa baba yake yaani Mungu ili kutuandalia makao ya milele baada ya kumaliza kuishi hapa duniani, kuna maisha mengine tutakwenda kuishi ambapo kuna maeneo mawili ambayo ni mbinguni na jehamanu. Bwana Yesu amekwenda kutuandalia makao yetu ya kudumu mbinguni na baada ya kutuandalia mahali atarudi tena kuja kutuchukua, Bwana Yesu kristo ilibidi amwombe Mungu ili amtume roho mtakatifu kwa ajili ya kupata maongozi sahihi kutoka kwake.Kuonyesha njia sahihi ya kuendea, kutukumbusha, kutushauri,kutuonya na kutufundisha kweli yote ya Mungu ambayo tunapaswa kuifahamu katika maisha yetu. Unapookoka na kumpa Yesu kristo maisha, Roho mtakatifu anafanya makao ndani yako na akishafanya makao katika maisha yako kila kitu kinakuwa chini ya maongozi yake, atakuwa anakushauri katika mambo yote na kikubwa zaidi unapokea Roho saba za Mungu katika maisha yako Isaya 11;2” Na roho ya BWANA atakaa juu yake ,roho ya hekima na ufahamu,roho ya ushauri, uweza ,roho ya maarifa na kumcha Bwana.” Roho hizi saba za Mungu zitakuwa ndani yako na utendaji wake wa kazi utadhihirika wazi wazi kwa watu wote kwamba unaye Roho wa  Mungu ndani yake. Roho wa Mungu anapoingia ndani yako anakupa hekima,ufahamu, ushauri, uweza, maarifa na kumcha Bwana. Unapofanyika mwana wa Mungu kila kitu katika maisha yako kinabadilishwa kabisa na mambo yote ya zamani yanabatilishwa ,yanaondolewa na unaanza mwanzo mpya kabisa pamoja na Bwana Yesu .2 kor 5; 17 Hata imekuwa mtu akiwa ndani ya Kristo amekuwa kiumbe kipya, ya kale yamepita tazama Yamekuwa mapya.” Unapompokea Yesu Kristo maishani mwako unaanza upya na anayetupa nguvu za kuanza upya ni roho mtakatifu ambae atakuwa anarejeza na kuumba kwa upya kila ambacho adui ameharibu ndani yako wakati ambao ulikuwa nje ya uwepo wa mungu. Roho wa Mungu anakupa ujasiri ndani yako wa kuanza upya.
Itaendelea …………………………………..

No comments