Highlights

MAJIRA YA KUJILIWA KWANGU.


MAJIRA YA KUJILIWA KWANGU.

Kwa kila jambo kuna majira yake na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu".(Mhubiri 3:1)
-Mungu anafanya kila kitu kwa majira yake ktk maisha yetu,tukiangalia Mwanzo 18:10 malaika walimwambia Sarah atapata mtoto wa kiume majira yaleyale mwaka unaofwata kama alivyoambiwa na malaika wa Bwana. Mwanzo 21:1 Mungu alitimiza neno lake alilomwambia Abrahamu kupitia wale malaika,Sara alijifungua mtoto wa kiume sawasawa na neno la Bwana.

KUJILIWA NI NINI?
Kujiliwa ni nyakati ambazo Mungu anakuwa halisi katik maisha yetu. Katika maisha ya wakristo wengi huwa na hizi hatua (Phases) tatu nazo ni
-kabla ya kuokoka.
-Baada ya kuokoka.
-Baada ya kujiliwa na Mungu.
Tukichambua kila hatua:

-Kabla ya kuokoka.
Hapa bado mtu hajampokea Bwana Yesu kama Bwana na mwokozi wa maisha yake.

-Baada ya kuokoka.
Hapa mtu anaamua kumkabidhi Kristo maisha yake ili awe Bwana na mwokozi wake.Watu wengi huishia katika stage hii ndio maana unaona mtu ameokoka lakini hamna improvement from point A to point B ktk maisha yake mfano mafanikio ktk elimu, uchumi n.k

-Baada ya kujiliwa na Mungu.
Kufikia level hii mtu anahitaji kuwa na mahusiano yenye nguvu au ya ukaribu sana na Mungu k.v Abrahamu ambaye ni mfano mzuri wa biblia. (Luka 19:41-44) inaonyesha watu wengi tunaangamia kwa sababu hatujui majira ya kujiliwa kwetu.
N.B Inahitaji mahusiano ya ukaribu sana na Mungu ili kujua majira ya kujiliwa kwetu.

MAMBO 3 MUHIMU YANAYOHUSIKA KTK KUJILIWA KWETU.
-Mahusiano yetu na Mungu.
-Meeting point yetu na Mungu.
-Tabia zetu (Attitude)
1)Mahusiano yetu na Mungu.
-Mahusiano yoyote yale huwa na levels (hatua) mfano mzuri k.v Uchumba ambapo watu hao wawili siku moja hutarajia kufikia level ya ndoa (marriage).
Vilevile kujiliwa kwetu na Mungu kunategemea mahusiano yetu sisi na yeye (Mungu).
-Kuna level ukifika hauhitaji kuomba ili Mungu ashuke inatokea automatically. Yohana MT 9:31, Warumi 8:31.
2) Meeting point yetu na Mungu.
-Ukishalocate your spiritual point usiiachie as long as una neno la Bwana hapo  (Zaburi 46:10) hapo ndipo Mungu atakapoinua karama yako hapo ndipo utakapopokea muujiza wako na hapo ndipo wengine watamuona Mungu kupitia yale anayotenda maishani mwako.
-Kuna baadhi ya watu bado hawajatambua meeting point yao na Mungu hivyo hutoka kanisa moja kwenda lingine wakilitafuta neno la Mungu,na miujiza hivyo humzuia Mungu kulocate their spiritual adress na hivyo hawajiliwi na Mungu katika maisha yao.Inatupasa kumuomba Roho Mtakatifu atuongoze kutafuta meeting point na Mungu.
 3)Tabia zetu  (Attitude)
-Kuna tabia nyingine zinamzuia Mungu kutujilia katika maisha yetu .(Wagalatia 5;19-21),tabia kama wivu, hasira,fitina,ugomvi,uasherati...n.k.
Inatupasa kujua maeneo yetu ya udhaifu na kumuomba Mungu atusamehe na kuyaondoa hayo madhaifu yetu ili aweze kutujilia ktk maisha yetu .Zab 51:1-3.
SWALI NA JIBU
Nifanye nini ili niweze kuepukana na hizi attitude
Ukishajua udhaifu wako ni vema kuwa na tabia ya kuomba toba mbele za Mungu mara kwa mara ili akusaidie kuepukana nao na pia jiepushe na mazingira yanayokufanya kuwa dhaifu.
-Ukisoma Zaburi ya 51 Mfalme Daudi alijua udhaifu wake na hio ndio sala yake ya toba mbele za Mungu,mstari wa 3 amesema "maana nimejua mimi makosa yangu na dhambi yangu i mbele yangu daima".

No comments