Highlights

UHUSIANO BINAFSI NA ROHO MTAKATIFU.



UHUSIANO BINAFSI NA ROHO MTAKATIFU.
Ninakusalimu katika jina la Bwana wetu Yesu Kristo. Ninapenda kumshukuru Mungu kwa kutupatia neema ya kujifunza somo hili wiki hii ambalo ni mwendelezo wa somo la juma lililopita tuliangalia namna roho mtakatifu anavyofanya kazi ndani yetu . Siku ya leo tunakwenda mbele kidogo na kuona namna gani kijana anaweza kuwa na uhusiano binafsi na Roho mtakatifu

   Maana ya uhusiano binafsi ni hali ya kuwa na uhusiano wa peke yako kama mtu mmoja au mtu binafsi na sio kundi la watu au kuwa na ukaribu, undugu wa karibu sana na Roho mtakatifu. Neno la Mungu linasema  Yohana 14; 16-18 Nami nitamwomba Baba baba naye atawapa msaidizi mwingine ili akae nanyi hata milele, ndiye Roho wa kweli ambaye ulimwengu hauwezi kumpokea kwa sababu haumwoni wala haumtambui ;bali ninyi mnamtambua maana anakaa kwenu ,naye atakuwa ndani yenu. sitawaacha yatima naja kwenu. Neno la Mungu hapa linatuambia kuwa “…bali ninyi mnamtambua maana anakaa kwenu ,naye atakuwa ndani yenu” neno la Mungu limetumia nafsi ya wingi kwa sababu alikuwa anaongea na wanafunzi wake ila Roho mtakatifu anakaa ndani ya mtu binafsi ndio maana neno linasema naye atakuwa ndani yenu. Akiwa na maana kwamba kila mtu binafsi atakuwa na Roho mtakatifu.Hii ni ahadi ambayo Yesu Kristo aliitoa kabla ya kupaa kwenda kwa baba yake kutuandalia makao. Ni ahadi yake kwetu kila mmoja wetu kuwa na Roho mtakatifu. Baada ya kuokoka unampokea Roho mtakatifu ili aweze kukusaidia kuishinda dhambi na dunia.

Ni maombi yangu kila kijana atamani kuwa na uhusiano na Roho mtakatifu kwani hakuna uhusiano wowote ulio bora kama uhusiano wa mtu binafsi na Roho mtakatifu. Kijana mkristo anapokuwa na Roho mtakatifu ndani yake hatapata shida kuitafuta sauti ya Mungu, hatakuwa mbishi katika kuifuata kweli ya Mungu kwani kwanzia ndani yake atakuwa anaongozwa na sauti ya Mungu Roho Mtakatifu. Na Roho Mtakatifu anamshuhudia binafsi na anaielewa sauti ya Mungu inayosema nae ndani yake na anaitii. Vijana wengi na wakristo wengi kwa ujumla wamejikuta wakihangaika kila kona kutafuta kuisikia sauti ya Mungu kupitia watu wangine na kusahau kuwa wao pia Mungu anasema nao kupitia Roho Mtakatifu na wanashidwa kumtii au wanadhania kuwa ni hisia zao tuu au ni mawazo yao. Nakuhakikishia kuwa hiyo sauti unayoisikia ndani mwako ikisema na wewe ndani yako hiyo ni sauti ya Mungu Roho Mtakatifu.Isaya 30; 20b-21”…..lakini waalimu wako hawatafichwa tena, ila macho yako yatawaona waalimu wako,na masikio yako yatawasikia neno nyuma yako likisema njia ni hii ifuateni……..” Roho mtakatifu ni mwalimu na kama ilivyo kazi ya mwalimu ni kumwongoza mwanafunzi katika njia ambayo ni sahihi na pale mwanafunzi anapokosea mwalimu anamwadhibu na vivyo hivyo na Roho matakifu kama maandiko yanavyosema mwalimu huyu, Roho mtakatifu atatuwa dhahiri na tutaona utendaji kazi wake kwa macho yetu na kwa masikio yetu tutaisikia sauti ,sauti ikisema na kutuelekeza njia sahihi ya kuifuata kama mtu binafsi bila kushinikizwa katika chochote.
     
   Tunapaswa kuwa na Roho Mtakatifu ndani mwetu kama mtu binafsi. Ile hali na mazoea ambayo wakristo wengi tumekuwa nayo ya kuamini kuwa Mungu anasema na watumishi wa madhabahuni pakee sio sahihi ila kila aliyempokea Yesu maishani mwake na kumkiri kwa kinywa chake Roho matakatifu anakaaa ndani mwake na kama Roho mtakatifu anakaa ndani mwake basi atakuwa anampa maongozi na maonyo sahihi kutoka kwake binafsi. Na pale Roho mtakatifu anapokuwa ndani mwako na ikafikia hatua kuwa unamsikia na kukitii kile anachokushauri basi kutoka hapo inaonyesha namna unavyozidi kukua na kukomaa kiroho.

     Na haya ndio mapenzi ya Mungu anatamani kutuona kunakua kutoka katika utoto na kuwa watu wazima. Huku ndiko kuukomalia wokovu. Tuna kila sababu ya kuuimarisha uhusiano wetu na Roho mtakatifu kuliko uhusiano mwingine wowote, wakristo wa leo tumekuwa kutitumia nguvu nyingi na gharama kubwa sana kuimarisha uhusiano wetu na watumishi wa Mungu ili kusikia Mungu akisema nasi kupitia wao sio kwamba nataka kupinga uhusiano huo ila napenda kukwambia Uhusiano wa kwanza na wa muhimu kuliko mwingine wowote ni uhusiano wako binafsi na Roho mtakatifu kwa sababu mtumishi wa Mungu hawezi kukuwambia kila kitu unachopaswa kufanya kwani ana kundi kubwa la kuhudumia. Unaweza ukaona Mungu amekuacha au amekusahau katika mapito unayokumbana nayo na ukajikuta ukikimbizana na watumishi wa Mungu kila kona kwa ajili ya kupata msaada lakini usifanikiwe kwa sababu Mungu atakataka uwe na uhusiano binafsi na yeye na ndipo atakaposema na wewe. Unapokuwa na uhusiano na Roho mtakatifu atakufunulia mambo mengi sana yaliyosirini. Na ataweza pia kuwafunulia na watumishi wa Mungu mambo yako na wakaweza kukusaidia na ukavuka kwa ushujaa mkubwa katika majira unayopitia

No comments