Highlights

NAMNA GANI ROHO MTAKATIFU ANATENDA KAZI NDANI YANGU.



MAISHA YA KIJANA MKRISTO NA WOKOVU.

Ninakusalimu katika jina la Yesu Kristo Bwana wetu, kipindi kilichopita tulipitia maisha ya wokovu ambapo tuliangalia Roho mtakatifu anavyofanya kazi ndani yetu. Siku ya leo ninatamani kuendelee mbele kidogo na kuangalia kwa kina ni kwa namna gani Roho mtakatifu anatenda kazi ndani yetu kama watoto wa Mungu. 

·         Roho mtakatifu hutupa amani na uhuru. 2 kor 3;17 “Basi ‘Bwana’ ndiye Roho ,walakini  alipo Roho wa Bwana ndipo penye uhuru”.Roho mtakatifu anapokuwa ndani yako ndani yako unakuwa na uhuru wa kimungu wenye mipaka,uhuru huu unatokea ndani ya mtu mmoja mmoja na baadae eneo la kijografia linakuwa na uhuru na amani ya Kristo. Kuna watu wakati wote wanaonekana wana hofu na huzuni na hata ukijaribu kukaa karibu nao kujua kwa nini wako katika hali hiyo unakosa jibu, jibu ni kuwa hawana Roho wa Mun gu ndani mwao

·         Kutusaidia kutambua dhambi. Roho mtakatifu anapofanya makazi ndani mwetu anatushuhudia au anashuhudia ndani mwetu pale tunapofanya kinyume na mapenzi ya Mungu. Anatupa kukosa amani na hali ya kujiona mkosaji inakuja kwa kasi sana ndani ya mwamini na hii ni kumtaka mtu huyo kuacha kabisa kuendelea kutenda hicho alichokuwa anakitenda au ni kumtaka atubu na kurejea tena kwa Bwana Yesu kwa ajili ya ondoleo la dhambi zake.

·         Anatuwezesha kutubu na kujuta pale tunapokosea. Roho mtakatifu anatupa kuwa na hali ya majuto ndani yetu na hali hii inatujia pale tunapotenda dhambi na Roho mtakatifu anapokuwa anakuletea hali ya majuto ndani yako au anapokuwa anasema na wewe mara nyingi na ukashupaza shingo yako, sauti hiyo hukaa kimya ndani yake na haitakuwa inasema na wewe tena, mfano mzuri ni watu wanaofanya matendo ya kikatili na ya kinyama kama kunyanyasa watu au vitendo vya mauaji ambavyo havina utu na huruma ndani yake, watu wanaojishughulisha na matendo haya Roho wa Mungu anakuwa hayupo ndani yao na wamemzimisha kwa kutoisikiliza sauti na maonyo yake 1wathes 5;19 “Msimzimishe Roho.”Roho mtakatifu anapokushuhudia unapokuwa umefanya jambo ambalo sio sahihi na ukakataa kumtii mara kwa mara unakuwa umemzimisha roho mtaktifu ndani yako na neno la Mungu limetutaka tusimzimishe Roho mtakatifu ndani yetu na njia pekee ya kutokumzimisha ni pale anapokushuhudia kwamba umekosea uwe na majuto na tubu mbele za Mungu ili usamehewe.

·         Kutusaidia katika kuomba warumi 8;26 “Kadhalika Roho naye hutusaidia udhaifu wetu kwa maana hatujui kuomba jinsi itupasavyo, lakini Roho mwenyewe hutuombea kwa kuugua kusikoweza kutamkwa”. Binadamu wote ni dhaifu hatujui kuomba ipasavyo kwa maana kwamba maombi yetu huwa yana makosa na mapungufu kadha wa kadha na  Roho mtakatifu pekee ndie anayeweza kutuombea ipasavyo.Yeye anajua mahitaji yetu ya muhimu kwa wakati huo tunapokuwa tunaomba wakati kwa jinsi ya mwili tunakuwa tunamwomba Mungu vitu kwa ajili ya kujiinua,kusifiwa na wenzetu na wakati mwingine kwa ajili ya kuwaumiza wengine ila pale tunapoomba kwa kuhitaji msaada wa roho mtakatifu . Mungu Roho mtakatifu hutuombea kwa kuugua kusikotamkika na kila haja tunayohiitaji roho mtakatifu anatusaidia kutuombea na wakati mwingine yale ambayo shetani amekusudia juu yetu kwa siri kupitia kuomba kwa msaada wa roho mtakatifu anakusaidia kuzijua hila za adui shetani na kuzikataa kupitia Roho mtakatifu.

·         Kutuwezesha kuomba kwa muda mrefu. Unapokuwa na Roho mtakatifu anakufundisha namna ya kuomba na atakuongoza katika maeneo tofauti tofauti ambayo utaweza kuyaombea wakati hata haukuwa umejiandaa kuyabeba maeneo au mahitaji hayo katika maombi. Kama kila ukiomba umekuwa maneno yanakukaukia au wakati mwingine unasahau mambo ya kuombea ebu badilisha namna yako ya kuomba na anza kuomba kwa kumwalika roho mtakatifu ndani yako awe kiongozi wako katika kuomba na utaanza kuona kuomba kwako kuna matunda na kuna mabadiliko ukilinganisha na ulipokuwa unaomba hapo kabla , unapookoka maombi yako pia yanapaswa kuwa na kupiga hatua sio pale ulipokuwa jana ndio hapo hapo tukija kesho kutwa tunakukuta hapo, kunapaswa kuwa na matokeo na mabadiliko chanya kila siku katika wokovu wako na katika maisha yako ya wokovu.

·         Kutupa ushikira na Mungu Ushirika kwa tafsiri nyingine ni umoja au ukaribu baina ya wahusika au urafiki pale Roho wa Mungu anapokuwa ndani yako atakusaidia kuweza kuwa na ushirika mzuri na Mungu Baba na Mungu mwana Yesu kristo.. 2 kor 13;14 Neema ya Bwana wetu Yesu kristo na upendo wa Mungu Baba na ushirika wa Roho mtakatifu ukae nasi sote sasa na hata milele.

Kwa mawasiliano zaidi
Simu 0654444433
         0624006533

No comments