Highlights

SERVANTHOOD LEADERSHIP IN 21ST CENTURY/KIONGOZI MTUMISHI KARNE YA 21

SERVANTHOOD LEADERSHIP IN 21ST CENTURY/KIONGOZI MTUMISHI KARNE YA 21

Kwanza kabisa Mtumishi ni kiongozi ambaye lengo lake kubwa ni kusaidia.
Utumishi unaoongelewa hapa ni ule wa kushirikiana na watu moja kwa moja kwenye kufanya kile mnachotakiwa kufanya. Sio kukaa na kuagiza hiki afanye uyu alafu wewe ume relax.Ni ushirikiano wa pande zote mbili zinazohusika hapo mbele kidogo tutaona sifa zake.
Swali ni je?Tunaweza tukapata kiongozi wa aina hii karne hii ya 21??
Karne yenye mambo mengi na taarifa nyingi ambazo tunaaminishwa kiongozi anatakiwa awe wa aina fulani???
Jibu ni Ndio inawezekana kabisa kuwa na kiongozi mzuri karne hii ya 21.

Kama wakristo tunaunganishwa na kupewa ukamilifu na Yesu unaoweza kabisa kutupa kiongozi ambaye hana sifa potofu ambazo tunazisikia na tumezoea kusikia kwamba ni lazima kiongozi awe nazo.

Luke 22:25_27
Akawambia wafalme wa mataifa huwatawala na wenye mamlaka juu yao huitwa wenye fadhili. 26.Lakini kwenu ninyi sivyo,bali aliye mdogo na mwenye kuongoza kama yule atumikaye ? 27. Maana aliye mkubwa ni yupi? Yeye aliyeketi chakulani au yule atumikaye?Siyo yule aketie chakulani ?Lakini mimi kati yenu ni kama atumikaye.

Kama Yesu mwenyewe alihudumu hata sisi tunayo nguvu na uwezo wa kuhudumu vizuri kama Yesu alivyofanya.Kutumika ni kazi inayotaka usiwe dictator.unatakiwa uwe tayari kuwaongoza watu. Kushirikiana nao katika kila jambo. Tuna mfano wa viongozi ambao tumewaona wakishirikiana na watu vizuri na kufanyika baraka.Kiongozi huyu tunaemsaidia anaweza akawa ni kiongozi wa kuhudumu kanisani, hata sehemu nyingine mbalimbali.

Kiongozi hatakiwi kuwa mtu wa kuchukulia anaowaongoza advantage ( you shouldn't take advantage of the people you are leading)
1peter 5:2 Lichungeni kundi la Mungu lililo kwenu,na kulisimamia, si kwa kulazimishwa,bali kwa hiari kama Mungu atakavyo, si kwa kutaka fedha ya aibu , bali kwa moyo. Ukiwa mtumishi unayehudumu sawasawa na mapenzi ya Mungu kwako title (cheo) hakitakupa shida. Utaichukulia kama nafasi ambayo unatakiwa kuitumia ili kutimiza mapenzi ya Bwana.

ZIFUATAZO NI SIFA KUU TANO ZA  MTUMISHI TUNAYEMZUNGUMZIA LEO

1. Servant Heart / Moyo wa kitùmishi 
Kuwa mtumishi anayeenda na mapenzi ya Mungu karne hii 21 unatakiwa uwe na moyo wa kitumishi.(Wito)

2. Meekness/ Upole
Hesabu 12:3
Inatuambia Musa alivyokuwa mpole sana zaidi ya wanadamu wote waliokuwa juu ya uso wa nchi.Lazima utakutana na watu wa aina mbalimbali na wenye mambo mbalimbali. Unatakiwa uwe mpole ili kuweza kukaa sawasawa na mapenzi ya Mungu

3. Humility/ unyenyekevu
Mathayo 18:4 Basi yeyote ajinyenyekesheye mwenyewe kama mtoto huyu, huyo ndiye aliye mkuu katika ufalme wa mbinguni. Unyenyekevu ni kila kitu. Hata Yesu alikuwa mnyenyekevu.

4. Sacrifice and selflessness/  Anayejitoa na asiye mbinafsi
Yohana 15: 13

5. Faithfulness/  mwaminifu
1korinto 4:2
Hapo tena inayohitajiwa katika mawakili ,ndiyo mtu aonekane kuwa mwaminifu Kiongozi lazima awe mwaminifu,Ni vizuri ukawa mwaminifu kwa kila jambo, uhaminifu sio kwa vitu tu hata kwa watu unaowahudumia. 

Hitimisho
Utumishi ni uchaguzi(choice)Lakini commitment inahitajika when you decide to be a leader.

1korinto 9:19
Maana ingawa nimekuwa huru kwa watu wote, nalijifanya mtumwa wa wote ili nipate watu wengi zaidi. 

 Imetafsiriwa na Dada Dorosela Kimaro.

No comments