Highlights

KEYS TO GREATNESS/FUNGUO ZA UKUU.

KEYS TO GREATNESS/FUNGUO ZA MAFANIKIO au UKUU.


Sisi sote ni watoto wa Mungu na tumeumbwa kwa sura na mfano wa Mungu. (aliye mkuu kuliko vitu vyote).Na kwa kila mtoto wa Mungu amepewa uwezo wa kuwa mkuu. Sisi watoto wa Mungu ni zao/tunda la Mungu wetu aliye mkuu, na tumeumbwa kwa namna ya pekee.
Zab:139:14
"Nitakushukuru kwa kuwa nimeumbwa kwa jinsi ya ajabu yakutisha, Matendo yako ni ya ajabu na nafsi yangu yajua sana."

UWEZO NI NINI?
NI ILE NGUVU ALIO NAYO MTU JAPO YAWEZA KUWA HAIJATUMIKA.
Ni nguvu iliyofichika.
Ni ile namna au hali ambayo mtu yakupasa uwe japo bado haijadhihirika katika ulimwengu wa mwili.(umbali mtu anatakiwa kuufikia/kwenda japo bado hajafanikiwa kufika).
Tunazidi kufundishwa kuwa; Uwezo ni yale yote Mtu anaweza kuyafanya japo bado hajayafanya/hajafikia. Uwezo si kile Kitu mtu kashafanya LA HASHA! Kwa maana mara nyingi watu wengi huridhishwa na kuvutiwa  na yale wameshafanya/ama kufanikiwa  na kusahau kuwa wanauwezo  wa kufanya makubwa zaidi.
 Hivyo tukiwa tungali hai tujue kuwa tuna uwezo wa kufanya mambo makubwa  na makuu sana katika ulimwengu huu,kwa ajili ya kizazi cha sasa na cha baadae.

Ili kuufikia ukuu/ama mafanikio yetu makubwa funguo zifuatazo yatupasa kuzizingatia na kuzitekeleza;

UFUNGUO  WA MAARIFA/UFAHAMU:
Tunaambiwa kuwa adui Mkubwa wa mwanadamu  ni ujinga na nyenzo  kuu ya uharibifu wa maisha ya mwanadamu ni ukosefu wa maarifa/ufahamu. 
Hosea 4:6 maandiko yanasema; 
"Watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa;Mimi nami nitakukataa wewe usiwe kuhani kwangu mimi;kwa kuwa umeisahau sheria ya Mungu wako,mimi nami nitawasahau watoto wako."
Hivyo basi ili tuweze kufikia ukuu/mafanikio katika maisha Yetu funguo ya kwanza ni maarifa,tupende kujifunza na kupata maarifa kwa njia mbalimbali,mf kusoma vitabu na kujifunza kwa waliofanikiwa.

Usione Shida  wala aibu kuuliza kwa kitu usichokifahamu.Kuwa na bidii katika kujifunza.Endapo Mtu utaona shida katika kujifunza/kutafuta maarifa, usimlaumu Shetani kwa kutofanikiwa kwako maana Huna maarifa ya kuufikia ukuu/mafanikio,wala kuanguka kwako usilaumu mtu yeyote maana nyenzo kuu ya kuanguka kwako ni Ujinga.

TUKISOMA MAANDIKO MATAKATIFU;
Daniel 9:2 Katika mwaka wa kwanza wa kumiliki kwake, Mimi Daniel kwa kuvizosoma Vitabu,Nalifahamu hesabu ya miaka,ambayo  neno la BWANA lilimjia Yeremia nabii,ya kuutimiza ukiwa wa Yerusalem Yaani miaka sabini.
Tunaona hapo Daniel kupitia kusoma vitabu aliweza kupata maarifa ya kuhesabu  miaka iliyobakia ya kuwa utumwani. Kuna wakati Mwingine katika safari ya kutafuta maarifa binadamu wanaweza kusema mengi na kuwa na maoni kadha wa kadha juu yako,LAKINI SONGA MBELE NA USIRUDI NYUMA.
Kwa maana ni Mungu pekee ndie anakujua wewe,hakuna binadamu anayeweza kukwambia ama kukuamlia maisha yako.Maoni ya binadamu juu yako ni ubatili Mtupu hivyo hayawezi kubadili nguvu na uwezo ulionao.

UFUNGUO NO.2.
KUBALI MAJUKUMU/WAJIBIKA.
Usiridhike na mafanikio ama hali ulionayo  sasa, KUBALI  kuwajibika zaidi na zaidi.
Zaburi:71:21 inasema"Laiti ungeniongezea ukuu,Urejee tena na kunifariji Moyo. 
Hapo tunaona kuwa mtu anatamani kuwa mkuu zaidi na zaidi,Hivyo usibweteke na kuridhika mahali ulipo leo,unauwezo  wa kuwajibika na kufanya makuu zaidi.

UFUNGUO NO.3
JIWEKEE MALENGO; 
Tengeneza Malengo yanayotekezeka, yapange kwa vipaumbele na uyatimize .
Weka Muda Maalumu (time frame) kwa kila lengo lako.mf.wiki,mwezi,mwaka n.k.WEKA MIKAKATI ITAKAYOKUSAIDIA KATIKA UTEKELEZAJI WA MALENGO YAKO KWA MAANA UKUU AMA MAFANIKIO HUWAPATA WATU WENYE NIDHAMU NA WALIO SERIOUS NA KITU WANAFANYA AMA WANAPANGA KUFANYA.  Na katika kutimiza malengo yako hakikisha kila unachofanya unakipa umuhimu na kutochukulia vitu as usual.

UFUNGUO NO 4.
KUMBATIA NDOTO,MAWAZO NA MAONO  YAKO.
Hapa inashauriwa usiwe kigeu geu, Leo una kile Kesho kingine,"stick to one thing at a time" Hakuna mafanikio au ukuu mtu anaweza kufikia bila kuwa na maono,ndoto na mawazo.Fikiria(imagine/pata picha) kuhusu ukuu/mafanikio yako baada muda fulani  Mf.unataka kuwa na familia bora na watoto wazuri ni lazima uwe na maono na ufuatilie maono yako hatua kwa hatua bila kuchoka wala kukata Tamaa. Mfano wa ndoto tunaona kupitia Mwanzo 37:5-8
"Yusufu akaota ndoto, akawapa ndugu zake habari,nao wakazidi kumchukia, akawaambia ,tafadhalini, sikieni ndoto hii niliyoota.Tazama Sisi tulikuwa shambani tukifunga Miganda, Kumbe!mganda wangu,ukaondoka ukasimama,Na Tazama Miganda yenu ikazunguka ikainama mbele ya mganda wangu.Ndugu zake wakamwambia Je,kweli utatumiliki sisi?Nawe utatutawala sisi?Wakazidi kumchukia kwa ajili ya ndoto yake na maneno yake."

Tunaona Yusufu anaota ndoto ya utawala lakini anapowashirikisha nduguze wanamchukia,Yamkini mimi na wewe tuna ndoto na kuna watu tumewashirikisha, na badala ya kusapoti ndoto zetu wanachukia na kutaka kutuangamiza,LAKINI NIKUTIE MOYO KUWA KILA KILICHOKIKUU HUPITIA MAGUMU.Mfano ni dhahabu  haiwezi ng'aa bila kupita katika Moto.Shikilia ndoto na maono yako na ufanyi kazi.

FUNGUO NO.6
JENGA MAHUSIANO YENYE TIJA
Kama unataka kuwa Mkuu/kupata mafanikio ni lazima uambatane na waliofanikiwa/waliofanikiwa, Mf.mtoto mdogo hawezi kuwa na tabia njema endapo company anayocheza au kushinda nao hawana maadili mazuri.
MAANDIKO MATAKATIFU;MITHALI 13:20 inasema;
Enenda pamoja na wenye hekima,nawe utakuwa na hekima,bali rafiki wa wapumbavu ataumia. "Tunaona maandiko  matakatifu yanatuonyesha namna mtu anaweza kuwa kulingana na watu anaoambatana nao.
 Hivyo basi katika kujenga mahusiano,unayo nafasi ya kuwa na mahusiano na watu unaowapenda na wanaokupa hamasa ya kufanya juhudi zaidi ili kufikia mafanikio yako.

Swali la kujiuliza kabla hujaanzisha mahusiano ama urafiki:
Kwanini uwe na mahusiano na watu wasio na malengo yoyote katika maisha? Kwanini uwe na mahusiano na mahusiano na watu wanaotaka kubaki kama walivyo /wameridhika?
Maandiko(Mithali 27:17) pia hapa yanasema"Chuma huona Chuma, Ndivyo mtu auonavyo Uso wa rafiki yake."Wapendwa,nataka leo tuanze kufanya tathmini juu ya marafiki tulionao,  hata ikitubidi kubadili uelekeo kwa ajili ya marafiki zetu.

UAMINIFU.
Hapa tunahimizwa kuwa waaminifu na kile unachotamani kuwa.
Mfano;kwa Mtu Anayetamani kuwa mwandishi Mashuhuri wa vitabu ili aweze kufikia hicho anachotamani cha kwanza ni lazima awe na Imani itakayomsukuma kufanya bidii katika kufikia hiyo level anayotamani awe.MAANDIKO MATAKATIFU KUTOKA MARKO:9:23 inasema"Yesu akamwambia  Ukiweza!Yote yawezekana kwake aaminiye."
MARKO 10:27 "Yesu akawakazia macho akasema,kwa wanadamu haiwezekani bali kwa Mungu sivyo, maana yote yawezekana kwa Mungu."
Maandiko haya yanatuonyesha jinsi Imani yako ni nyenzo kuu katika kufikia chochote unachotamani kuwa.Maana Imani uliyo nayo ndio ikupayo nguvu ya kutenda na kujitoa zaidi.


UFUNGUO NO.7 HUDUMIA/FANYA HUDUMA.(SERVICE)
Huwezi kuwa mkuu ama kufanikiwa hadi pale utakapojitoa kwa ajili ya wengine.MAANDIKO YAMETUONYESHA MFANO MINGI,juu ya watu waliojitoa na kufanya huduma na ndipo walipokuwa wa kuu.  Yusufu alikuwa kijakazi hatima yake ilikuwa ni Uwaziri.Saul alimhudumia babae. Elisha  alimhudumia Bwana wake Eliya.Yesu Kristo Mwenyewe alijitoa kwa Mungu baba na kwa wanadamu pia na ndipo alipokuwa Mkombozi  wa ulimwengu.
Hivyo katika kutoa huduma  kwa uaminifu na moyo mkuu yamkini ndipo muujiza wako ulipo,fanya jitihada katika kuwahudumia wengine haijalishi utakutana na magumu yapi ama gharama kubwa kiasi gani,maana pia katika huduma ndipo Unyenyekevu wako utapoongezeka na penye Unyenyekevu siku zote Pana mafanikio makubwa.

 UFUNGUO 8.TOA SHUKRANI.
Katika Maisha yako na safari yako ya mafanikio,jifunze kutoa Shukrani,kwanza kwa Mungu wetu kwa jambo lolote Liwe jema ama baya 
Pili kwa wanadamu waliokushika mkono kwa namna yoyote ile,Neno ASANTE lina nguvu sana wapendwa,na kama haujawahi kulitumia au linakuwa gumu kwako jifunze kuanzia Leo. pia kuna namna mbalimbali za kutoa shukrani zako na shukrani ni njia ya kuomba tena na tena,Hivyo basi  tunahimizwa kuwa watu wa shukrani ili kufikia mafanikio yetu katika maisha.
 IN SUMMARY;FUNGUO ZA MAFANIKIO YAKO:
TAFUTA MAARIFA.
WAJIBIKA/KUBALI MAJUKUMU.
WEKA MALENGO.
KUMBATIA NDOTO,MAWAZO NA MAONO YAKO.
KUWA NA IMANI.
JENGA MAHUSIANO YENYE TIJA.
TOA  HUDUMA/HUDUMIA. 
KUWA NA SHUKRANI/TOA SHUKRANI.



Imetafsiriwa na Dada FLORA MASHIMBA

1 comment:

  1. Asante mtumishi Magreth kwa kushare. Mungu akaibari kazi ya mikono yako ukainuliwe kwa viwango vingine. Utukufu hadi utukufu.

    ReplyDelete