Highlights

YOUNG LEADERS AND BOOKS / VIONGOZI VIJANA NA USOMAJI WA VITABU


YOUNG LEADERS AND BOOKS / VIONGOZI VIJANA NA USOMAJI WA VITABU 

Viongozi ni wasomaji wa vitabu?
Kuna msemo unaosema sio kila wasomaji wote wa vitabu ni viongozi, lakini kila viongozi ni wasomaji. Not all readers are leaders but all leaders must be readers.


Kusoma vitabu inakuboresha kujua lugha na maendeleo kwa maisha ya kibinadamu.

Kadri unavyosoma vitabu ndivyo unavyojua au kufahamu mambo mengi, na kadri unavyojua ndivyo unavyowezapata matokeo.

Katka vitabu unaelimika na kuwa muelewa,unajua umuhimu wa mafanikio ktk maisha. Hosea 4:6 Watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa....

Usipokuwa msomaji hupati maarifa usipopata maarifa unaangamizwa na wenye hila. Kama mpendwa husomi Neno ili upate maarifa atakuja mtu na mstari wake atakuyumbisha tu...hutakuwa na nguzo ya kusimamia

TUONE WASOMI 3 WA KWENYE BIBLIA

1.DANIEL
......mimi Danieli, kwa kuvisoma vitabu, nalifahamu hesabu ya miaka, ambayo neno la BWANA lilimjia Yeremia nabii, ya kuutimiza ukiwa wa Yerusalemu, yaani, miaka sabini.Daniel 9:2
Kwa kusoma vitabu aliweza kugundua hili neno la Bwana

2. YESU KRISTO
17 Akapewa chuo cha nabii Isaya, akakifungua chuo, akatafuta mahali palipoandikwa,

18 Roho wa Bwana yu juu yangu,Kwa maana amenitia mafuta kuwahubiri maskini habari njema.Amenituma kuwatangazia wafungwa kufunguliwa kwao,Na vipofu kupata kuona tena,Kuwaacha huru waliosetwa,
19 Na kutangaza mwaka wa Bwana uliokubaliwa. Luka 4:17-19

3.MTUME PAUL
Ujapo ulilete, na vile vitabu, hasa vile vya ngozi. 2 Tim 4:13
Mtume Paul anaagizia aletewe vitabu ili asome, inaonyesha yeye ndie wa kwanza kuwa na Maktaba ya vitabu.
Anza leo kuweka maktaba ya vitabu nyumbani mwako,nunua vitabu,usome vitabu
 Bill Gates na rafki yake Paul Allen kwa kusoma Magazeti waliweza kugundua na kuanzisha Computer project.
Miongoni mwa watu waliofanikiwa sanasana viongozi ni wasomaji wazuri wa vitabu. Kuna baadhi ya misemo inayoweza kutusaidia;

a) Kitabu ni zawadi unayoweza kufungua tena na tena.
Garrison Keillor

b) Uelewa ni daraja katika matatizo na matumaini. (Uelewa tunaupata kwa kusoma)
Kofi Annan

c) Kitabu kinachomletea mtoto tabia ya kusoma ni kizuri kwake.
Maya Angelou

d)Kusoma itolewe kama zawadi kwa mtoto na sio kwa lazima au kazi.
Kate DiCamillo

e) Kusoma ni mazoezi ya akili.
Richard Steele
 Kwa kusoma unapata faida nyingi.....Kujua historia 
Mathayo 12:3
Akawaambia, Hamkusoma alivyotenda Daudi, alipokuwa na njaa,yeye na wenziwe?
Hawa watu wangekuwa wamesoma wasingemnung'ukia Yesu kuwa wanafunzi wako wanavunja na kula siku ya sabato
1 Tim 4:13 Ufanye bidii katika kusoma na kuonya na kufundisha.
Nami nakusihi leo ufanye bidii ktk kusoma,utajua ahadi za Mungu,utasimamia imani yako,utaweka tumaini la kweli katika Kristo.

Imeandaliwa Dada Furaha Mosha na kuwekwa hapa na Magreth Gift Mushi




No comments