Highlights

KEY TO ACADEMIC SUCCESS/ FUNGUO ZA KUKUSAIDIA KUFAULU MITIHANI


KEY TO ACADEMIC SUCCESS/ FUNGUO ZA KUKUSAIDIA KUFAULU MITIHANI

Mungu anapenda sisi tupate maarifa. Na maarifa haya tunayapata kwa namna mbalimbali na moja wapo ni kwa kwenda shuleni. Tunapokwenda shuleni tunaenda kupata maarifa mapya na kuongeza ufahamu.

Isaya 11:2[2]Na roho ya BWANA atakaa juu yake, roho ya hekima na ufahamu, roho ya shauri na uweza, roho ya maarifa na ya kumcha BWANA;
Roho hizi 07 za Mungu zinakaa ndani mwetu. Kama zilivyotabiriwa kuwa juu ya Yesu Kristo. Tunapaswa kuwa na bidii katika kutafuta maarifa na siku tutakayoacha kutafuta maarifa ni siku tunaingia kaburini. Tuko hapa pia kupata maarifa.

: FUNGUO 05 KWA UFAULU MZURI
1. MALENGO /FOCUS
Kuna mambo mengi sana yanayotushawishi sisi kama vijana. Na yanaweza kutuvuta sisi tuyape Muda wetu. Na kama mwanafunzi hauwezi kufaulu mitihani yako kwa kuwa katika mazingira yanayokusumbua na kukuangaisha.  Wanafunzi wengi wanaenda shuleni na akili zao hazipo shuleni. 
Huwa unapata matokeo mazuri kwa kile ulicholipia gharama kubwa.  Kuna kanuni ya Pareto inasema 20% ya kile unachofanya inakupa 80% ya matokeo. Unapaswa Kujua kwa 20% na kuweka MALENGO yako hapo

 2. DETERMINATION/KUAMUA

Unapaswa kuamua. Kuna vitu vingi unaweza kuvifanya kuwa visingizio vyako. Ila tunapaswa kuvuka visingizio vyetu. Tumekuwa watu wa kusingizia mifumo na wazazi wetu. Wisingizio sio suluhisho. Unapaswa kukiacha visingizio na kuchukua hatua.

3. KUWA NA BIDII/ HARD WORK. 
Mbele ya kila mafanikio kuna sura ya kufanya kazi kwa bidii. Hakuna kitu kinatokeaga kama hakuna mtu aliyefanya kazi kwa bidii. Vitu havitokei tuu kwa sababu tunakiri na kuvitamka tuu ila vinatokea kwa sababu pia ya kufanya kazi kwa bidii kukiri na kuamini pekee haitoshi. "There is no a substitute of hard work "
Hakuna kitu kinatokea kama kama hakuna mtu atakayekifanya.  Hata kwa wanafunzi hauwezi kufaulu mitihani kwa kuamini kwamba utafaulu tuu. Ila ni lazima usome kwa bidii.

4. KUSOMA/ STUDYING
Danieli 9:2[2]katika mwaka wa kwanza wa kumiliki kwake, mimi Danieli, kwa kuvisoma vitabu, nalifahamu hesabu ya miaka, 

Kuna nguvu katika kusoma vitabu. Kuna utajiri mwingi sana umefichwa kwenye vitabu. Tunapaswa kusoma vitabu kupata majibu ya maswali mengi tunayokuwa tunajiulizaga.Hii point nitakuja kuielezea zaidi Katika somo la Nguvu iliyoko katika kusoma vitabu ambayo nitatuma hapa katika somo lijalo.

5. KUMWAMINI MUNGU. 
Hauwezi kufanikiwa bila msaada wa Mungu unamwitaji Mungu kila wakati katika maisha yako ya masomo kama mwanafunzi uwako shuleni. Mtangulize Mungu katika kila jambo unalotamani kumwona Mungu amakutangulia.

Imeandaliwa na Mwl. Magreth Gift Mushi  Mawasiliano 0654 444433

No comments