Highlights

MAXIMIZING YOUTHFUL SEASON / KUTUMIA VIZURI KIPINDI CHA UJANA


MAXIMIZING YOUTHFUL SEASON / KUTUMIA VIZURI KIPINDI CHA UJANA

Tukisoma Muhubiri 3:1
Inasema kila jambo lina majira yake. Na kuna kuna wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu.
Kulingana na kichwa cha habari hapo juu, tunajulishwa kwamba biandamu kama binadamu ni mtu wa wakati. Kuna wakati ulikuwa mtoto, umekuwa mdada au mkaka sasa utakuwa mama au baba kesho na  utazidi kuendelea na wakati mwingine kadri Mungu atakavyokujalia.
Kipindi cha ujana ni kipindi chenye mambo mengi mno, unakuwa na nguvu, mitazamo mbalimbali,ndoto nyingi za vitu mbali mbali. Unakuwa pia fresh unakuwa pia na idea nyinginyingi ambazo unaziwaza. Unakuwa unatamani kujaribu kila kitu unachoona kinakufaa. Unakuwa na wigo mpana sana wakufanya na kutatua mambo mbalimbali.

Ukiwa kijana sio kwamba ndo mahali pa kustarehe, sio mwisho wa basi. Bado safari inaendleea zaidi na zaidi.

Kwa hiki kipindi kinaweza kuwa kizuri au kibaya kwako kama hutakitumia vizuri.Sasa kuna mambo ya kufanya ili kumaximize mda wako wa ujana inabidi utambue mambo yafuatayo:

MAMBO YAKUELEWA NA KUFANYA UWAPO KATIKA KIPINDI CHA UJANA.
1. Upo kwenye kipindi cha kuelewa mda/Season of understanding the times 
Unachotakiwa kufanya ni kumueka Mungu wa kwanza, huwezi kumweka Mungu ukashindwa kitu. Huu ni mda wa wewe kama kijana kukaa na Mungu vizuri ndiyo baadae yako itakapokuwa njema. Tunaambiwa tuutafute kwanza ufalme wa mbinguni ndivyo na mengine yote tutakapozidishiwa.Kwa hiyo ni vizuri ukaelewa hiki kipindi ni cha kumtanguliza Mungu kwa kila jambo. 

2.Ni mda wa ndoto na maono /Season of dreams and Visions
Ni kipindi kila kijana anakuwa na ndoto na maono mengi ambayo anatakani yaje yatimie baadae. Kama Yusufu alivyoota ndoto yake ya kuja kutawala badae,haikutimia kesho yake ilichukua mda na ilitaka uvumilìvu na utii kwa Mungu kwa hali ya juu sana. Tuwe na ndoto na maono lakini pia tuwe na uvumilivu na utii wa Neno la Mungu ndivyo tutakavyofanikiwa.

3. Season of learning lessons/ Ni mda wakujifunza
Elimu inatakiwa ikuandae kuja kufanikiwa. Lakini pia wewe kama wewe unafanya nini kwa kutumia elimu unayopata sehemu mbali mbali? Huu ndo mda wa kujifunza vitu vingi ambavyo baadae vitakuja kutusaidia.Tusome vitabu tuudhurie training etc ambayo vitatujenga na kutupa maarifa zaidi na zaidi.

5. Season of development/ Ni kipindi cha maendeleo
Hapa ni kujiandaa na badae yako/uzee. Huu ndo mda wakujijenga kiuchumi, kifamilia na kila kitu kikipita kipindi cha ujana hakirudi. Ni vyema ukatumia vizuri ujana ili uweze kuendelea na njia yakuendelea inaanzia kwa Mungu. 

NJIA KUU MBILI ZAKUKABILIANA NA KESHO YAKO
1. Expectation of rewards is the result of preparation .Kama usipojiandaa leo usitegemee kupata mema uko mbeleni.

2. Fear of repercussions is the result of lack of preparation ,Kwahiyo ni vizuri tukajiandaa vyema.

Mahali pa kujiandaa 
1. Spiritual Preparation/ maandalizi ya rohoni
Tusome 1Yohana 2:14 Nadhani hamna asiyeelewa jinsi ya kujiandaa kiroho
2. Mental preparation/kujiandaa kiakili.Tafuta maarifa mbali mbali yatakayokupa kujifunza mambo yatakayopanua akili yako na kukupa maarifa mbali mbali. Jiandae kiakili kwamba hapa kwenye ujana sio mwisho wa maisha,utapita na stage nyingine itakuja. Kwa hiyo ni vyema tukawa tayari kiakili
3. Physical Preparation/ maandalzii ya kimwili
Fanya mazoezi ili kumaintain mwili wako. Ishi vizuri sawasawa na maagizo Mungu aliyoagiza tuyaishi.
5. Social preparation/ maandalizi ya kijamii
Hapa ni vizuri uka socilize na watu mbali mbali, ndo kipindi chako cha kujamiiana na watu mbali mbali.Lakini pia maarifa yanaitajika ili kujua namna gani ya kurelate na watu unaoitaract nao.


YOTE YA YOTE UKUMBUKE TU HUWEZI KUWA KIJANA MARA MBILI. KIPINDI CHA UJANA NI ZAWADI TOKA KWA MUNGU. TUUTUMIE UJANA VIZURI KWA HEKIMA NA MAARIFA TULIYOPEWA NA MUNGU.

IMETAFSIRIWA NA DADA DOROSELA KIMARO

No comments