Highlights

UFUPISHO KWA LUGHA YA KISWAHILI KUTOKA KATIKA KITABU CHA BIBLE SENSE OF GETTING INTO MARRIAGE


UFUPISHO KWA LUGHA YA KISWAHILI KUTOKA KATIKA KITABU CHA BIBLE SENSE OF GETTING INTO MARRIAGE {KUINGIA KWENYE NDOA KWA MTIZAMO WA KIBIBLIA}.KILICHOANDIKWA NA DAVID OYEDEPO.



Kitabu kinaelezea jinsi au namna ya kufanya ili ndoa yako iwe yenye furaha na amani. Ndoa imeanzishwa na Mungu ili kuwafuraisha wanadamu. Ndoa ni kitu kizuri kinachounganisha watu pamoja, nikimaanisha kwamba mume anapoungana na mke pamoja katika kujenga familia tunaona kwamba undugu unakua zaidi.



Kwa hiyo ili uwe na ndoa njema ni lazima ndoa yako misingi yake ianzie kwa Mungu,ili ndoa iwe ndoa lazima MUNGU asimame katikati tukijua kwamba yeye ndie mpaji wa vipaji vyote, yasiwe ni mawazo yako tuu au hisia  ukahitimisha kuwa huyu ndiye, mambo yakiwa mabaya hata Mungu hatakusikiliza maana hukufata anavyotaka Yeye. Nanukuu kutoka sehemu katika kitabu hiki imeandikwa kwamba



 “Marriage is a good thing established by God, for the benefit of man. But to enjoy the benefits, it must be entered into as God intended it to be”.

 (Ndoa ni kitu kizuri kilichoanzishwa na Mungu, kwa manufaa ya mwanadamu. Lakini ili kufaidi manufaa, lazima ufanye kama Mungu alivyopanga). Hivyo ndoa ni kitu kizuri Mungu akisimamia.



Kutengeneza ndoa njema huanza na wewe mwenyewe ukikubaliana na changamoto zote na kujua jinsi ya kuzitatua  ili kupiga hatua mbele zaidi, kuna msemo unajulikana sana kwamba “Usikosee kuoa/kuolewa” Je, walikua na maana gani kusema hivyo ..ni wazi kuwa walijua changamoto zitokanazo na hilo.



Pia unapotafuta mwenzi haitokei tu ulalapo au uotapo ndotoni ni akili yako inayokuongoza na kukuwezesha kutambua nani atakayekufaa kuliendesha gurudumu la maisha yenu, hivyo ndoa ni kitu kizuri ambacho MUNGU akiwa ndani mwake hudumu daima.



»Kabla ya ndoa lazima mchunguzane ili kila mmoja amjue mwenzie vema, sio mnakutana siku moja mkapendana wiki mkataka ndoa ikafungwa...aisee matatizo yakitokea nani alaumiwe?? hapo ndipo utaona kila moja anamlaumu mwenzie na kujiona yeye ni mwema asie na kosa hata kama yeye ndo mwenye makosa.



Kumtafuta mwenzio 

  • Lazima awe mwamini. Hakuna  makutano kati ya mwenye dhambi na mcha Mungu. KUMBUKA: ni rahisi sana mwenye dhambi kumshawishi mcha Mungu kutenda dhambi, kuliko mcha Mungu kumgeuza mwenyewe dhambi.



  • Hapa unatakiwa uwe makini Weka vigezo vyako, kuwa makini na mtu unayeingia katika mahusiano naye. Sio rohoni tu au kimawazo. Na amesema vizuri kabisa usianze kuang'ang'ana na mtu asiyeamini maana ni rahisi sana wewe kurudi nyuma kuliko kuendelea mbele.  Hata kama ni nzuri kiasi gani au unatamani iwe ndo hiyo hiyo kama sio mwamini ni bora ukaacha ili ufate mapenzi ya Mungu. Ametolea mfano wa agano Mungu aliloingia na Abrahamu kwamba wasioe nje ya ukoo wao.Pia sisi tumesisitizwa sana kutokuangalia au kutafuta wale wasio njia moja na wewe. Ni bora uue mapenzi yako kuliko uyafate baadae mambo yashindikane. Hata Mungu hatakusikiliza maana Yeye pia analiangalia neno lake apate kulitimiza.



»UCHUMBA

Mara nyingi kwa kipindi hiki watu wengi hatufuatilii hii hatua, tunakurupuka halafu tunakuja  kujutia baadae. Ni lazima kuwa katika uchumba kwa muda ili tuweze kuchunguzana na kujua tabia zetu kiundani zaidi, ili kama mtu hajapendezwa na mambo anayoyafanya mwingine, tuweze kurekebishana, kabla hatunaingia kwenye ndoa. Uchumba unasaidia sana watu wanajuana vizuri.Hiki ni kipindi cha kuchunguzana sasa ili  kuimarisha uhusiano wenu, je mnaendana, tabia zenu zikoje (unapenda nini, upendi nini, unafuraishwa au hufuraishwi na nini, unapendezwa, hupendezwi na nini n.k) Kupitia hayo unaweza tambua anakufaa/ hakufai.

»Maombi pia hubadilisha usichoke kuomba omba kwa Imani nawe utapokea kwa imani

»MITHALI 18:22 Apataye mke apata kitu chema; naye ajipatia kibali kwa BWANA.

    Alpha ana nyimbo inaitwa Yes...kuna verse inasema “he who finds a wife finds a good thing, give me wisdom to protect this love…(Yeye apataye mke, apata kitu chema, nipe hekima ya kulinda penzi hili) ni kweli kabisa kwamba apataye mke apata kitu chema.

   »Ndoa si kwa ajili ya wavulana na wasichana ni kwa ajili ya wanaume na wanawake tena waliojiandaa vema.

  »Ndoa ni chaguo na si kulazimishwa/kutumia nguvu. Ili ndoa iwe ndoa lazima kuwe na makubaliano baina ya watu wawili wenye msimamo mmoja wa kuanza maisha yao mapya kwa pamoja vilevile mkiishi maisha yenu kama nyie, msiruhusu kuishi maisha ya kuangalia wengine wanaishije mtafeli. Tunapoona ndoa nyingi zinafeli kwa sababu hiyo ya kuangalia akina fulani wanaishije, daima usiishi maisha ya kuangalia akina fulani wanaishije,wanakula nini, wanavaaje...ishi maisha yenu nanyi mtabarikiwa haijalishi ni maisha gani mliyonayo, daima penda kujua njia za kukupandisha viwango kutoka ulipo kuelekea juu zaidi ya ulipo hiyo ndio njia sahihi kuliko kutafuta mbinu za kupindua wengine.

  • Ndoa inajengwa na mume na mke wenye kutambua wajibu wao kama ilivyo agizo la Mungu mwenyewe, mume kumpenda mke na mke kumtii mume, Waefeso 5:24-25

Ndoa inajengwa na watu wenye muelekeo unaofanana, compatibility Ndoa lazima iwe ni ya makubaliano, Ndoa ni chaguzi na sio shuruti, kila mtu ana haki ya kuamua. Kipindi cha uchumba ndio kipindi cha kujua mbivu na mbichi, yaani  ni kipindi cha kutafuta ukweli kwa sababu uchumba unavunjika na sio ndoa na ni kipindi pia cha kuaminisha upendo wako kwa mwenza wako, pia na kubakia ni ya watu wawili, wazazi au marafiki huwa wanafuata baadae. Katika wakati huu, una haki ya kukataa, kukemea kuhoji na sababu, tabia vitu ambavyo huviamini na ambavyo havikusaidii na kumpa Mungu utukufu.



Makubaliano

 Baada ya kumpata ambaye unaona analingana na viwango vyako ni lazima pia mkubaliane. Hauwezi kuongozana tu kama hamjakubaliana. Ni lazima akubaliane na viwango ulivyonavyo.Na hutakiwi kuogopa kuonyesha msimamo wako. Weka wazi unachotaka kama akikubalina anaweza utajua kama ndo yeye au sio. Nimesoma na kitabu cha Mwalimu Mwakasege cha kabla ya kuolewa anasema uwe wazi kabla hamjaenda kwenye hatua nyingine. Usipoteze muda kuremba remba mtu au kuficha kusema nini unataka, hata kama ni namna ya kuchana nywele ni lazima wote mkubaliane. 



Kuchunguzana kwa pande zote mbili

Lazima umchunguze mwenzio vizuri sana ili kujua kila kitu kabla ya kuingia kwenye ndoa. Na haitakiwi kuwa miezi tuu au muda mfupi sana. Mnatakiwa mjuane vizuri ili mkiingia kwenye ndoa kusiwe na tofauti. Mwandishi amesema ndoa nyingi zina shida kwa sababu hapa wengi wanaona madhaifu lakini hawasemi wanajipa moyo au kuendelea. Na pia hutakiwi kusikiliza ndugu, marafiki n.k  ni wewe utaishi naye uko ndani usiku na mchana kwahiyo ni vizuri ukafanya uchunguzi uridhike wewe sio ndugu au yeyote. Kama hujaridhika na mtu ni bora umwambie tu ukweli. Katika hali  iliyo tulivu si kwa kumtumia ujumbe wala kumpigia simu, ni kukaa ana kwa ana  na kuambiana tu ukweli. Kabla ya kukurupuka na kuenda kutambulisha kwa wazazi, ndugu utajikuta tu wewe ni wa kutambulisha /kutambulishwa kila mara na familia pia itakuchoka.



Muendelezo

Kuendelea ni hatua nyingine ambayo baada ya kufahamiana ukaona tabia, madhaifu yenu mnaweza kuchukuliana basi ni jambo la ndugu familia na wazazi kujua pia lakini kipindi hiki yaani unakutana na mtu siku mbili wazazi hawamjua ila WhatsApp wako wote wamesha mjua sio kwa kurusha huko. Ukiwa hivyo utaonyesha wangapi maana hamkuja mtaachana tuwe makini. Kama vingine uko juu viko sawa ndo uendelee na hapa. Kama haviko sawa usiendelee maana matatizo yatakayokupata wewe ndiyo utakayehangaika maana maamuzi uliyafanya wewe. Ni lazima uwe makini. 



Kulindana

Hiki bado ni kipindi cha uchumba kwa hiyo ni vizuri mkalindana kwa kuombeana ili msije mkaanguka dhambini. Ni lazima uweze kujichunga ili usimsababishie mwenzio kuanguka pia. Hasa kwa wanawake, sisi hapa ndio wa kuwasaidia wanaume maana sisi ndio tunayachochea zaidi mpaka unakuta watu wanaanguka kwenye uzinzi. Ni vizuri tuweze kujizuia na kujitunza.Utakavyomsaidia mwenzio ndivyo mtakavyoeweza kulifikia lengo salama. 



Kukataa

Hapa ni kukataa tabia unazoona zitakuja kuleta shida uko mbeleni. Hata kama vimetoka kwa ndugu ni lazima ukatae na kuweka vigezo ambavyo huko mbeleni hazitaleta shida kwenye ndoa yenu. Ni bora kurekebishana hapa kuliko kuja kuleta ugomvi huko baadae. Hii ni hatua ya kuangalia mambo gani ambayo yanaweza kuharibu ndoa yenu msipokuwa makini. Ndoa ni watu wawili na sio jamii nzima inayokuzunguka msije mkaruhusu wengine kufanya shauri kwenye ndoa yenu. Hata kama ni wazazi mkaona kwamba hapa mnamkosea Mungu ni bora na iyo ndoa isiwepo kabisa maana makabila mengine wana mila ambazo kiukweli hazivumiliki kuliko umkosee Mungu ikose hiyo ndoa.



Jiandae kwa ajili ya wakati ujao.

Andaeni mazingira mnayoyaendea baada ya ndoa, makazi malazi, sio mabinti tunategemea kuolewa na mwanume si ana pesa, mie sihitaji kufanya lolote hapana hata binti nawe tengeneza mazingira yako kama mke na mama mtarajiwa  sio hata kupika mboga unaanza mpigia mama yako utapika nin,i hapana nasi tujiweke tayari kuna mambo inabidi tujifunze kabisa. Hapa ni tusikurupuke kufanya vitu. Ni lazima ujipange na kujiandaa vyema maana mnaenda kuanza familia. Mahitaji yataongezeka. Ratiba zako hazitakuwa tena kama za sasa hivi. 

Kama kila kitu kipo sawa kuanzia hatua ya kwanza ndio uendelee kufunga kabisa pingu za maisha.Kama hapana, kumbuka uchumba unavunjika. Usilazimishe vitu vitokee. Acha mapenzi ya Mungu yatimizwe. 



Utambulisho

Mkiwa mmeridhika   na mmeshajuana, utambulisho ufuate,  ili iweze kuwa rasmi baada ya hapo

sasa mnaweza mkachukua hatua ya kwenda mbele ya altare. Kuweka nadhiri zenu mbele za Mungu na familia ikiwa mashahidi kuwa sasa mke na mume rasmi.



NB:

Kuna mambo ambayo mkiyafanya wakati wa uchumba mkiyapeleka kwenye ndoa lazima ndoa itayumba napo tuweni makini sana tuweni na mipaka.

Mungu awabariki sana na Roho Mtakatitu atuongoze kupata Mume mwema katika maisha yetu aliye sahihi kwetu.




NYONGEZA:

Kuna mambo 5 unayopaswa kuyafanya ili uwe na kujipenda na kujiamini:

1. Kubali nini au nini kilikuumiza katika kipindi kilichopita. 

2. Muombe Mungu au tafuta msaada wa kisaikolojia ili uweze kuponywa moyo wako kutokana na maumivu yaliyokupata 

3. Jikumbushe kuhusu tabia, sifa na mambo mazuri uliyonayo au uliyowahi kuyafanya. 

4. Waepuke watu ambao wapo kwa ajili ya kukuangusha au kukufanya ujione una kasoro. 

 5. Jikubali na ujipende, tafuta vitu unavyovipenda kuhusu wewe, nini kinakufanya uwe tofauti na wengine?   



KIMEFANYIWA UFUPISHO NA

 MWANDISHI MAGRETH GIFTH MUSHI PAMOJA NA MABINTI WA HUDUMA YA

 A LADY WITH A PURPOSE.

 KWA MAWASILIANO ZAIDI

255 654 444433


@ June 2019


Download Hapa

No comments