Highlights

MSICHANA MWOMBAJI NA MCHA MUNGU



Msichana unapaswa kuwa na tabia ya kuomba na kutafuta kuwa rafiki wa Mungu. Haya yanapaswa kuwa ndio maisha yako ya kila siku na sio matukio ya muda hasa ukiwa na shida.Usiombe pale tu unapoona mambo hayaendi sawa, hapana unatakiwa uwe mwombaji wa kila wakati na binti anayetafuta kufanya mapenzi ya Mungu nyakati zote, hii ndio tabia ya kiungu katika maisha ya binti aliyeokoka.

 Kuna vitu vingi sana hautaweza kuvipata kama hauombi na kama una konakona kwenye maisha yako. Na tambua kuwa baraka zako nyingi zipo magotini mwako na katika kumuishia Mungu (utakatifu), ni jukumu lako sasa kuingia magotini na kumwomba Mungu akusaidie kumtii Roho wake Mtakatifu anapokufundisha na kukushauri.Unapokuwa muombaji kuna vitu vingi Sana vitatendeka katika maisha yako na pia kuna mazingira ambayo Mungu atakuwa anakuepusha nayo kwani mwili wako unakuwa unahuishwa chini ya Mungu (Warumi 12; 1).

Mwanamke amchae Mungu ndiye atakayesifiwa.Mith 31; 10 Biblia imeshatupa muongozo hapa kuwa mwanamke anayemcha na kumsikiliza Mungu atasifiwa, kamwe mwanamke anayekaa na mashoga zake tu na kujadili mambo yasiyo na maana hatosifiwa daima, zaidi sana ni kujikuta unapata majeraha ya nafsi , viwango vyako viweke kwa Yesu pekee.









No comments